Monday, December 31, 2012

WALIOTUSUA BONGO MOVIES 2012

 


WAKATI leo tukiufunga mwaka 2012, Ijumaa Wikienda linakudondoshea listi ya waigizaji wakali wa filamu za nyumbani waliofanya jitihada kwa kupiga mzigo hivyo kuibuka kidedea sokoni kwa muvi nyingi na kujiingizia mkwanja mrefu (kutusua).
 
Wema Sepetu.
Ifuatayo ni orodha ya mastaa 10 ambao wamefanya vizuri na kuuza filamu nyingi kuliko wengine ndani ya mwaka huu.
 
JACOB STEVEN ‘JB’Huyu ni mwigizaji mkongwe kunako gemu la filamu Bongo. Kupitia kampuni yake ya Jerusalem, JB anakiri kuwa ndani ya mwaka huu amefanya kazi nyingi. Amecheza filamu 23 na zote zipo sokoni na zinafanya vizuri katika mauzo tofauti na mwaka uliopita. Unaikumbuka DJ Ben?
 
STEVEN KANUMBA
Marehemu Steven Kanumba alitisha sana mwanzoni mwa mwaka 2012, kila mwezi alitupia kitu sokoni. Alipofariki dunia Aprili 7, filamu zake zote ziligombewa kama njugu sokoni. Filamu zaidi ya 10 ziliuzwa kwa kipindi hicho, mpaka sasa ile ya Ndoa Yangu ambayo ndiyo ya mwisho kuigiza, bado inatamba sokoni.
 
MZEE MAJUTOMwanzoni King Majuto alitisha kwenye filamu na maigizo ya kuchekesha. Ijumaa Wikienda linamzawadia nafasi kwa kuwa kila kona zilipouzwa filamu kulikuwa na muvi aliyocheza na biashara ilifanyika. Unakumbuka ripoti ya kutisha ya utajiri wake iliyotokana na kazi yake ya uigizaji? Mzee yupo vizuri.
 
VINCENT KIGOSI ‘RAY’
Nafasi hii tunaitoa zawadi kwa Ray kwani kupitia kampuni yake na mwigizaji Blandina Chagula ‘Johari’, RJ Production, aliweza kutengeneza filamu takribani 10 ambazo zipo sokoni na nyingine hazijatoka hadi sasa. Mzigo wa mwisho ni Waves of Sorrow, uliotanguliwa na Sister Mary.
 
DOKTA CHENI
Jamaa alifanya poa sana sokoni. Alikimbiza na anakimbiza na muvi kibao ambazo bado zinagombewa, mzigo wake wa mwisho ni Majanga.
 
WEMA SEPETUKwa upande wa wanawake, mwanadada Wema ameonekana kuuza katika filamu kibao ndani ya mwaka huu kwani wengi wanavutiwa na muonekano wake, hali iliyosababisha kufanya kazi zaidi. Ndani ya mwaka 2012 alicheza filamu zaidi ya 13 za watu. Mwisho akacheza moja ya kwake ya The Super Star aliyoizindua kwa kishindo kwa kumdondosha Bongo staa wa Nollywood, Omotola Jalade.
 
IRENE UWOYAHakuwa nyuma katika kufanya kazi japokuwa kuna kipindi alionekana kushuka kidogo. Baadaye filamu za watu alizocheza na za kwake zilikamata soko ghafla na kuwa gumzo kila sehemu zilipouzwa.
 
JACQUELINE WOLPERIjumaa Wikienda linamzawadia nafasi hii mwanadada huyu kwani kupitia kampuni yake alifanikiwa kutengeneza filamu saba ambazo zipo sokoni na nyingine kibao alizoshirikishwa na watu ambazo hakumbuki idadi yake.
 
MONALISA
Mwaka 2012 ulikuwa wa mafanikio kwa mwigizaji huyu kwani alipata tuzo ya msanii bora wa kike ambapo alicheza filamu kibao za kwake na nyingine zipatazo tano alishirikishwa na watu.
 
ELIZABETH MICHAEL ‘LULU’Kabla ya kukumbwa na mkasa wa kuhusishwa kwenye kifo cha Kanumba, Lulu alifanya poa sana mwanzoni mwa mwaka huu. Akiwa mahabusu, hivi karibuni ilitoka filamu yake mpya inayokwenda kwa jina la Dangerous Girl inayofanya vizuri sokoni.
CHANZO; GPL

Mercy Johnson gives birth to baby girl

 

 
 
 
Mercy Johnson Okojie gave birth to a baby girl  in a hospital in the US. Got the news just now from the people in the hospital with her. Mother and daughter are said to be doing great. Big congrats to Mercy and her husband.

“SCENES ZA MAPENZI KWENYE FILAMU ZINAWAUMBUA WASANII WANAONUKA MIDOMO” – IRENE UWOYA

 


MSANII wa filamu anayejichukulia umaarufu bongo Irene Uwoya, amedai kuwa kuna baadhi ya wasanii wenye majina makubwa wanapenda kucheza filamu za mapenzi na uchezeana huku wakishindwa kuelewa kuwa wananuka midono na mara nyingine huwa wanavumulia pasipo kutoa ukweli huo.
Kauli kama ya msanii huyu iliwahi kutolewa na Janet Jackson kwenye filamu ya ‘Poetic Justice’ iliyozinduliwa mwaka 1993 akimtaka Tupac Shakur kupima  ukimwi kwani kuna kipande walitakiwa kuonekana wakipeana midomo kwani walicheza kama wapenzi ndani ya filamu hiyo, ndiyo kitu ambacho hata kwa wasanii wa kitanzania wanatakiwa kujifunza na si kukurupuka kupeana midomo..

Uwoya alisema kuwa kuna sehemu huwa wanakosea na kupeana midomo bila kupima afya kwani wapo wasanii wengine si wasafi na wananuka midomo huku wengine wakiwa wanatumia sana dawa za kulevya hivyo kuna hatari kubwa ya kuambukizwa magonjwa endapo wasipo chukua hatua.
Alisema kuwa wengine wanajijua walivyo lakini wanashindwa kujisafisha na kuwa katika hali nzuri badala yake ndani ya filamu wanaanza kupeanda kiss na kuchezeana bila kujua afya ziko vipi.

“Sasaivi naanza kuwa mkali kwa sababu endapo tukiendelea kuwa kimya tunaweza kujikuta magonjwa yanatukuta hivi hivi” aliongeza.
Hata hivyo msanii huyo aliwashauri baadhi ya wasanii wenye tabia za kupenda kupeana midomo ndani ya filamu wawe makini kwani huwezi jua ni ugonjwa gani anaoweza kupata, na kikubwa zaidi ni kupima kabla ya kazi kuanza ili kama kuna mtu mwenye tatizo apewe tiba mapema.

It’s Not Over Until You Win!

 

 
(1) No matter how bad life beats you up, stay in the ring and fight, never give up, fight for your dreams; Every champion was once a contender, Every success was once a dream. You have to start somewhere to get somewhere. Big dreams start with small steps. Keep fighting until you win
 
(2)Your ability to discipline yourself to do what you should, when you should, whether you feel like it or not, is one of the keys to becoming a person of excellence and living a life of success.
 
(3)How fast you start is not as important as how strong you finish. The hardest part of the race is just before the finish line; Stay strong and Never quit
 
(4)Assumptions kill relationships, procrastination kills dreams, and pride kills opportunities! Don’t let them murder yours
 
(5)Never sacrifice your FUTURE on the alter of your past; Your past is just a memory to learn from, a step to build on and not a path to return to; break free and stay free; the only way forward is forward! No one walks into the future constantly looking at the past
 
(6) The best time to do anything is now! Regret comes from not doing the things you know you could have done. Don’t let your future be filled with regrets. Be wise! Act now!
 
(7) Sometimes “good things” fall apart, so better things can come together! Don’t get worked up! Trust God’s plan not yours
 
(8)Excellence can be obtained if you, care more than others think is wise, risk more than others think is safe, dream more than others think is practical and expect more than others think is possible. Dare to be different.
 
(9)Your status gives you NO RIGHT to treat people like trash. You might be at the top, but you’re still under God! Stay Humble
 
(10) Be very aware of your worth. Some situations need you WAY MORE than you need them! Keep the ball in your court.”
 
#ChangeStartsWithYou!
 
~Ose~

Jessica Simpson tweets bare baby bump

 

 
 
Jessica Simpson is heavy again barely eight months after giving birth to her first child, Maxwell. The proud mum to be shared this photo on her Twitter page yesterday Sunday December 30th with the caption - 'bumpin and proud'.

Kim K and Kanye West expecting their first child

 

 
 
Kanye made this surprise announcement last night while performing at Revel in Atlantic City, New Jersey. Kanye said:
"Stop the music and make noise for my baby mama," referring to Kim, who was in the audience.
Shortly after Kanye shared the news, Kim's sisters, Khloe and Kourtney expressed their happiness via Twitter.
 
Kim is reportedly 12 weeks pregnant. So happy for her. Congrats to them!

Wednesday, December 26, 2012

Diamond, Dimpoz wafanya kufuru usiku wa X-Mass Dar Live.

 

…Chezea Diamond wewe!
Watu weweee: Kila mmoja akiwa na shauku ya kumpa mkono Diamond.
…Leka dutigite: Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe na Diamond wakiwapagawisha mashabiki kwa wimbo wa Leka dutigite.
Ommy Dimpoz ‘on da stage’!
Dimpoz na wasanii wake wakiwasha moto kuwakumbuka wapendwa wao waliotangulia mbele ya haki.
…Dimpooo…zzz: Umati ukipiga yowe wakati Ommy Dimpoz akifanya kufuru stejini.
…Platnumz hewani: Diamond akiwa amebebwa juu na madansa wake.
…Nataka kulewa, zikinipanda nimwage radhi.
…Nataka kulewa, lewa…: Diamond akiimba wimbo wake wa Nataka Kulewa.
…Nature ua… Nature ua… Nature ua..: Ndivyo Juma Nature alivyokuwa akienda sambamba kwa staili hiyo na mashabiki.
…Wanaume Halisi wakiendeleza libeneke ndani ya Dar Live.
Shakira akipelekeshana puta na Dimpoz stejini.
KR Muller akigonga mvinyo ndani ya mask.
…Zitto kazini: Siyo siasa tu, hata mistari mi mkali.
Kikosi cha Diamond Platnumz kazini.
Dimpoz na Shakira wakimwaga nyuki stejini.
Manjonjo ya madansa wa Dimpoz.
Diamond akiwachizisha mashabiki.
Madansa wa Dimpoz wakionyesha umahiri wao.
…Wakizidi kukonga nyoyo za mashabiki.
Zitto Kabwe akicheza kwenye kiti baada ya kunogeshwa na swagga za Dar Live.
Platnumz na dansa wake kama ‘The Wacko Jacko’.
Shughuli pevu ya Diamond na madansa wake.
…Waacheni watoto waje kwangu: Ndivyo allivyokuwa akichombeza Diamond wakati akitaka kumchukua mtoto huyu.
Platnumz akiipagawisha meza ya wageni waalikwa.
Waalikwa wakionyesha nyuso za tabasamu wakiongozwa na Mwasiti (wa pili kulia) na Prodyuza aliyetengeneza wimbo wa Leka dutigite, Tudi (wa tatu kushoto).
Prodyuza na Mwanamuziki mkongwe, Ally Mohammed ‘Baucha’ akikamua stejini.
…Nimpende naniii… Nimpende…: Wapambe “Wemaaaaaaaaaaaaa!”
Madansa wa Extra Bongo wakinogesha zaidi burudani za X-Mas ndani ya Dar Live.
Mpiga gitaa la besi wa Extra Bongo, Hosea Mgoachi akijiachia na shabiki jukwaani.
Pozi la Platnumz.
Wasanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya nchini Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Omary Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ usiku wa kuamkia leo wameweka historia kwa kufanya shoo ya aina yake ndani ya ukumbi wa kisasa wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam. Wasanii hao walisindikizwa na mkali Juma Nature na kundi lake la Wanaume Halisi, Msanii mkongwe Ally Baucha pamoja na Bendi ya Extra Bongo. Shoo hii imeletwa kwenu kwa hisani kubwa ya Serengeti Premium Lager na Vodacom – Wajanja wa Kujirusha.
(PICHA ZOTE : RICHARD BUKOS NA ISSA MNALLY / GPL)

Friday, December 21, 2012

VIDEO INAYOONESHA SHAMSA AKIJIFUNGUA YAZUA KIZAAZAA






VIDEO inayomuonesha msanii wa filamu Bongo, Shamsa Ford akijifungua imezua kizaazaa baada ya mtu asiyejulikana kuichukua bila ridhaa ya mhusika na kuisambaza kwa watu mbalimbali.


Shamsa Ford.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, rafiki wa karibu wa Shamsa alisema kuwa, video hiyo msanii huyo alirekodiwa kwa ajili ya kumbukumbu zake lakini ameshangaa kusikia kuna baadhi ya watu wanayo.
“Yaani video hiyo imezua kizaazaa, Shamsa anahaha kumjua aliyeisambaza lakini pia anahakikisha haiwafikiii watu wengine na vyombo vya habari kwani inamuonesha hatua kwa hatua akijifungua,” kilisema chanzo hicho kilichoomba hifadhi ya jina lake.
Baada ya kuzipata taarifa hizo, mwandishi wetu alimtafuta Shamsa ambaye alisema: “Kiukweli nimeumia sana, hiyo video ni kwa ajili ya kumbumbuku zangu, kwa nini mtu aichukue na kuisambaza bila ridhaa yangu? Imeniletea matatizo makubwa.

Monday, December 10, 2012

Jackline Wolper Amtambulisha Mchumba Wake Mpya Baada ya Kushindwana na Dallas




ALHAMISI iliyopita (Desemba 6, 2012), ilikuwa ni siku ya kuzaliwa ya Jacqueline Wolper, jioni yake ndani ya Synergy Lounge, Oysterbay, Dar es Salaam, alifanya bonge la pati, akiwaalika ndugu, jamaa, marafiki na majirani.

Mbele ya kila aliyehudhuria, Wolper alimtambulisha mchumba wake mpya ambaye amempiga bao, Abdallah  mtoro, ‘Dallas’ lakini akawaacha waalikwa na maswali lukuki pale alipogoma kumtaja jina.

Hakuishia hapo, akaomba mchumba wake huyo asipigwe picha hata ya kwenye simu, akisisitiza kuwa wana maana kubwa kuzuia hilo.


Mara nyingi mwenye fedha hata kama hasemi, vitendo vyake huongea, na kelele za jamaa huyo zilisomeka kwa herufi kubwa pale ulipowadia muda wa kumtuza ‘mtoto aliyezaliwa’ ambapo alimtuza cheni zenye thamani kubwa.

Wale waliomwakilisha jamaa huyo, hawakusema bei iliyonunuliwa, badala yake mmoja wao alitamka: “Cheni hizi zina thamani kubwa, kuliko zawadi yoyote ambayo inaweza kutolewa hapa.”

Cheni hizo ni mbili, moja ya shingoni na nyingine mkononi.


Mastaa kibao walihudhuria sherehe hiyo, kila mmoja alishangweka vya kutosha, huku misosi ikiwa siyo ya kuuliza, keki ilikatwa na kuliwa, shampeni zilifunguliwa na matukio mengine mengi ya kuvutia.

MC wa shughuli hiyo, Salum Mchoma ‘Chiki’, aliichangamsha sherehe na uwepo wa staa wa vichekesho, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’, ulisababisha mbavu za waalikwa ziteseke.

Wolper, alipomtangaza mchumba wake huyo, alizungumza kwa kujiamini na madaha ndani yake na kusababisha wegeni wengi washangilie, huku wachache wakipigwa na butwaa.

Mmoja wa mastaa waliopigwa na butwaa, alihojiwa na ripota wetu na akajibu: “Kiukweli nilishangaa, unajua maneno yaliyokuwepo ni kwamba baada ya kuachana na Dallas angefulia lakini leo imekuwa tofauti ndiyo maana nimeshtuka kidogo.”

Staa huyo , alipoona atatafsiriwa vibaya, akaongeza kama aliyekumbuka kitu: “Lakini naomba ieleweke mshtuko wangu ni wa heri. Nampenda Wolper na namtakia maisha mema na huyo mchumba wake.”


Wapambe waliokuwa na mchumba huyo wa Wolper, walizungumza kwa kishindo ukumbini: “Kama kuna mtu alikuwa na mategemeo kwamba huyu mrembo atapata shida, hayo mawazo aondoe kabisa.

“Tunajua kila kitu kwamba Wolper alikuwa na mtu ambaye alishindwa kumgharamia, kwa hiyo hapa kafika. Tutamhudumia vizuri sana.”

 Kwa mjibu wa Wolper, sherehe hiyo imegharimu shilingi 19,600,000.

“Nawashukuru sana marafiki zangu waliokuja kunisapoti kwenye sherehe hii maana nimejisikia faraja ambayo sikutegemea kuipata kwa leo.

“Nimetumia milioni 19 na laki 6 kwa ajili ya kuandaa sherehe hii ili niwaburudishe marafiki  na ndugu zangu, ingawa kwa haraka haraka wengi ukiwatajia fedha hii wataona ni nyingi ila waliyokuwemo ukumbini wenyewe wataamini maana vinywaji na vyakula vyote vilikuwa vikitoka humo humo na hatukununua nje.”

CREDIT: GPL

Rihanna blasts Chris Brown as he parties with Karrueche in Paris



Rihanna was very angry after she found out Karrueche Tran joined Chris Brown in Paris and partied with him on Friday night after his concert.

She took to twitter and sent out a series of angry tweets that seemingly were aimed at Chris. She tweeted- Examine what you tolerateClaps for the basic b**ches. See more below...

 
 
 

Chris Brown must have reached out to her to explain what Karrueche was doing with him in Paris because Yesterday night, Rihanna Tweeted a photo of herself lying in his arms with the caption,  
'Damn....... I miss my nigga #thuglife #BFFlif. See it after the cut...