Thursday, February 7, 2013

NDOA YA AUNT EZEKIEL "INAPUMULIA MASHINE"




KUMEKUWEPO na vijineno vya chinichini kuwa eti ndoa ya msanii maarufu wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel aliyofunga hivi karibuni na Sunday Demonte haipo na wabaya wake wamekuwa wakieneza taarifa hizo kwa kasi ya ajabu.
Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti, watu waliodai ni mashosti wa karibu wa staa huyo walisema wamebaini dalili za wazi kuwa ndoa yake imeyeyuka.
“Mimi ndiyo nawaambia sasa, kama mlikuwa hamjui ndoa ya Aunt haipo. Fuatilieni mtabaini ukweli wa hiki ninachowaambia.

“Nyie si mjiulize mbona tangu amerudi kutoka Dubai hajaenda tena kumfuata huyo mumewe? Si alisema amekuja kuweka mambo yake sawa kisha anakwenda kuifurahia ndoa yake, kiko wapi sasa?” alihoji mmoja wa wanyetishaji hao aliyeomba jina lake lisiandikwe gazetini.

Mwingine aliyekuwa mmoja wa waliofanikisha ndoa ya Aunt kwa kiasi kikubwa ambaye naye aliomba jina lake liwekwe kapuni alisema:
“Hata mimi nina mashaka na hii ndoa ya huyu mwenzetu, lakini iwe imevunjika, haijavunjika sisi haituhusu, kila mtu ana maisha yake bwana.”

Katika kujua ukweli wa madai haya, mwandishi wetu alimtafuta Aunt na alipotakiwa kulizungumzia hilo alisema:

“Tuna mipango yetu mimi na familia ndiyo maana Sunday yupo Dubai na mimi huku. Sipendi kuongelea mambo ya ndoa yangu magazetini lakini kwa kifupi ipo sawa.”

GLOBAL

Monday, December 31, 2012

WALIOTUSUA BONGO MOVIES 2012

 


WAKATI leo tukiufunga mwaka 2012, Ijumaa Wikienda linakudondoshea listi ya waigizaji wakali wa filamu za nyumbani waliofanya jitihada kwa kupiga mzigo hivyo kuibuka kidedea sokoni kwa muvi nyingi na kujiingizia mkwanja mrefu (kutusua).
 
Wema Sepetu.
Ifuatayo ni orodha ya mastaa 10 ambao wamefanya vizuri na kuuza filamu nyingi kuliko wengine ndani ya mwaka huu.
 
JACOB STEVEN ‘JB’Huyu ni mwigizaji mkongwe kunako gemu la filamu Bongo. Kupitia kampuni yake ya Jerusalem, JB anakiri kuwa ndani ya mwaka huu amefanya kazi nyingi. Amecheza filamu 23 na zote zipo sokoni na zinafanya vizuri katika mauzo tofauti na mwaka uliopita. Unaikumbuka DJ Ben?
 
STEVEN KANUMBA
Marehemu Steven Kanumba alitisha sana mwanzoni mwa mwaka 2012, kila mwezi alitupia kitu sokoni. Alipofariki dunia Aprili 7, filamu zake zote ziligombewa kama njugu sokoni. Filamu zaidi ya 10 ziliuzwa kwa kipindi hicho, mpaka sasa ile ya Ndoa Yangu ambayo ndiyo ya mwisho kuigiza, bado inatamba sokoni.
 
MZEE MAJUTOMwanzoni King Majuto alitisha kwenye filamu na maigizo ya kuchekesha. Ijumaa Wikienda linamzawadia nafasi kwa kuwa kila kona zilipouzwa filamu kulikuwa na muvi aliyocheza na biashara ilifanyika. Unakumbuka ripoti ya kutisha ya utajiri wake iliyotokana na kazi yake ya uigizaji? Mzee yupo vizuri.
 
VINCENT KIGOSI ‘RAY’
Nafasi hii tunaitoa zawadi kwa Ray kwani kupitia kampuni yake na mwigizaji Blandina Chagula ‘Johari’, RJ Production, aliweza kutengeneza filamu takribani 10 ambazo zipo sokoni na nyingine hazijatoka hadi sasa. Mzigo wa mwisho ni Waves of Sorrow, uliotanguliwa na Sister Mary.
 
DOKTA CHENI
Jamaa alifanya poa sana sokoni. Alikimbiza na anakimbiza na muvi kibao ambazo bado zinagombewa, mzigo wake wa mwisho ni Majanga.
 
WEMA SEPETUKwa upande wa wanawake, mwanadada Wema ameonekana kuuza katika filamu kibao ndani ya mwaka huu kwani wengi wanavutiwa na muonekano wake, hali iliyosababisha kufanya kazi zaidi. Ndani ya mwaka 2012 alicheza filamu zaidi ya 13 za watu. Mwisho akacheza moja ya kwake ya The Super Star aliyoizindua kwa kishindo kwa kumdondosha Bongo staa wa Nollywood, Omotola Jalade.
 
IRENE UWOYAHakuwa nyuma katika kufanya kazi japokuwa kuna kipindi alionekana kushuka kidogo. Baadaye filamu za watu alizocheza na za kwake zilikamata soko ghafla na kuwa gumzo kila sehemu zilipouzwa.
 
JACQUELINE WOLPERIjumaa Wikienda linamzawadia nafasi hii mwanadada huyu kwani kupitia kampuni yake alifanikiwa kutengeneza filamu saba ambazo zipo sokoni na nyingine kibao alizoshirikishwa na watu ambazo hakumbuki idadi yake.
 
MONALISA
Mwaka 2012 ulikuwa wa mafanikio kwa mwigizaji huyu kwani alipata tuzo ya msanii bora wa kike ambapo alicheza filamu kibao za kwake na nyingine zipatazo tano alishirikishwa na watu.
 
ELIZABETH MICHAEL ‘LULU’Kabla ya kukumbwa na mkasa wa kuhusishwa kwenye kifo cha Kanumba, Lulu alifanya poa sana mwanzoni mwa mwaka huu. Akiwa mahabusu, hivi karibuni ilitoka filamu yake mpya inayokwenda kwa jina la Dangerous Girl inayofanya vizuri sokoni.
CHANZO; GPL

Mercy Johnson gives birth to baby girl

 

 
 
 
Mercy Johnson Okojie gave birth to a baby girl  in a hospital in the US. Got the news just now from the people in the hospital with her. Mother and daughter are said to be doing great. Big congrats to Mercy and her husband.

“SCENES ZA MAPENZI KWENYE FILAMU ZINAWAUMBUA WASANII WANAONUKA MIDOMO” – IRENE UWOYA

 


MSANII wa filamu anayejichukulia umaarufu bongo Irene Uwoya, amedai kuwa kuna baadhi ya wasanii wenye majina makubwa wanapenda kucheza filamu za mapenzi na uchezeana huku wakishindwa kuelewa kuwa wananuka midono na mara nyingine huwa wanavumulia pasipo kutoa ukweli huo.
Kauli kama ya msanii huyu iliwahi kutolewa na Janet Jackson kwenye filamu ya ‘Poetic Justice’ iliyozinduliwa mwaka 1993 akimtaka Tupac Shakur kupima  ukimwi kwani kuna kipande walitakiwa kuonekana wakipeana midomo kwani walicheza kama wapenzi ndani ya filamu hiyo, ndiyo kitu ambacho hata kwa wasanii wa kitanzania wanatakiwa kujifunza na si kukurupuka kupeana midomo..

Uwoya alisema kuwa kuna sehemu huwa wanakosea na kupeana midomo bila kupima afya kwani wapo wasanii wengine si wasafi na wananuka midomo huku wengine wakiwa wanatumia sana dawa za kulevya hivyo kuna hatari kubwa ya kuambukizwa magonjwa endapo wasipo chukua hatua.
Alisema kuwa wengine wanajijua walivyo lakini wanashindwa kujisafisha na kuwa katika hali nzuri badala yake ndani ya filamu wanaanza kupeanda kiss na kuchezeana bila kujua afya ziko vipi.

“Sasaivi naanza kuwa mkali kwa sababu endapo tukiendelea kuwa kimya tunaweza kujikuta magonjwa yanatukuta hivi hivi” aliongeza.
Hata hivyo msanii huyo aliwashauri baadhi ya wasanii wenye tabia za kupenda kupeana midomo ndani ya filamu wawe makini kwani huwezi jua ni ugonjwa gani anaoweza kupata, na kikubwa zaidi ni kupima kabla ya kazi kuanza ili kama kuna mtu mwenye tatizo apewe tiba mapema.