Thursday, May 17, 2012

MAFISANGO AFARIKI KWA AJALI YA GARI

 KIUNGO wa kimataifa wa Rwanda, Patrick Mutesa Mafisango wa Simba, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo kwa ajali ya gari iliyotokea maeneo ya Tazara, Dar es Salaam. Mafisango amefariki kwa ajali ya gari akiwa anarejea nyumbani kwake, kutoka disko na kwa sasa mwili wke upo katika hospitali ya taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam.

Meneja wa Simba SC, Nico Njohole amethibitisha kifo cha mchezaji huyo na amesema hilo ni pigo kubwa kwa klabu hiyo. Mafisango aliyekuja nchini mwaka juzi na kujiunga na Azam kabla ya kuhamia Simba mwaka jana, alizaliwa Machi 7, mwaka 1987 Rwanda na kabla ya Tanzania alichezea APR ya Rwanda.

Mechi ya mwisho Mafisango kuichezea SImba ilikuwsa dhidi ya Al Ahly Shandy Jumapili katika hatua ya 16 Bora ya Kombe la Shirikisho, ambayo Simba ilitolewa kwa penalti 9-8, kufuatia sare ya jumla ya 3-3. Hadi anafariki dunia, Mafisango alikuwa ni tegemeo na jana tu Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geoffrey Nange Kaburu alisema kiungo huyo yupo kwenye mpango wa kocha wa kikosi cha msimu ujao.

Poleni wana Simba wote, pole kwa ndugu, jamaa na familia ya Mafisango. Bwana ametoa, Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe milele. Amin. Mungu iweke pema peponi Roho ya Marehemu.





Hivi ndivyo gari ya Marehemu Patrick Mafisango ilivyokuwa mara baada ya kupatwa na ajali na hatimae kupelekea kifo chake,Mwili wa Marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili.Tutazidi kufahamishana kadiri ya habari zitakavyokuwa zikiingia.
chanzo:kajunason blog

No comments:

Post a Comment