Tuesday, October 9, 2012

MWANAFUNZI AFANYA MTIHANI WA TAIFA WA KIDATO CHA 4 AKIWA WODINI MORO

 

Mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya Sekondari ya Alfa Germ, Morogoro, Jesca Kiliani (17) akifanya mtihani wa taifa akiwa wodi namba 7B  katika hospitali ya rufaa ya mkoa huo jana, baada ya kulazwa kufuatia kufanyiwa operesheni ya uvimbe.
MWANAFUNZI wa kidato cha nne katika Sekondari ya Alfa Germ, Morogoro, Jessica Kiliani (17), amelazimika kufanya mtihani wake wa kuhitimu elimu  hiyo akiwa wodini baada ya kufanyiwa upasuaji.
Hatua hiyo ilifikiwa baada ya mwanafunzi huyo, kuomba aruhusiwe kufanya mtihani huo licha ya kuwa  wodini akiugulia maumivu ya upasuaji aliofanyiwa na madaktari wa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa zaidi ya saa mbili na kulazwa katika wodi ya wazazi namba 7B.
Picha na KALULUNGA BLOG

No comments:

Post a Comment