Wednesday, October 10, 2012

WAREMBO WA REDD'S MISSTANZANIA 2012 WAKUTANA NA MH. LOWASSA MONDULI

 
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa akisalimia na Msimamizi (Matron) wa warembo wa Redd's Miss Tanzania 2012, Irene Karugaba wakati Warembo hao walipotembelea Nyumbani kwa Waziri Mkuu Mstaafu, Monduli ili Kupata Baraka zake. Mh. Lowassa aliwapokea warembo hao kwa furaha na kuzungumza nao machache juu ya mafanikio ya Mashindano hayo na Maendeleo ya Taifa letu la Tanzania.
 

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa akizungumza na Warembo wanaowania Taji la Redd's Miss Tanzania 2012 waliofika nyumbani kwake Monduli leo na kupata wasaa kwa kuzungumza nae mambo mawili matatu juu ya mafanikio ya Mashindano hayo na Maendeleo ya Taifa letu kwa ujumla.
 

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa na Mkewe Mama Regina Lowassa wakiwa kenye picha ya pamoja na Warembo wanaowania Taji la Redd's Miss Tanzania 2012 pamoja na Viongozi wa Kamati ya Miss Tanzania.

No comments:

Post a Comment