Showing posts with label NEWS ALERTS. Show all posts
Showing posts with label NEWS ALERTS. Show all posts

Friday, September 14, 2012

IKULU:Taswira mbalimbali za Ziara rasmi ya Rais Jakaya Kikwete Nchini Kenya


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwa katika hafla ya kutoa heshima zao na kuweka mashada ya maua kwenye Kaburi la Mwanzilishi wa Taifa la Kenya, Hayati Jomo Kenyatta jijini Nairobi Septemba 12, 2012 akiwa katika Ziara Rasmi ya Kiserikali (State Visit) ya siku tatu ambayo ni ziara yake ya kwanza rasmi nchini humo ingawa amefanya ziara kadhaa za kikazi nchini Kenya.
Rais jakaya kikwete akiweka shada la maua kwenye kwenye Kaburi la Mwanzilishi wa Taifa la Kenya, Hayati Jomo Kenyatta jijini Nairobi Septemba 12, 2012 akiwa katika Ziara Rasmi ya Kiserikali (State Visit) ya siku tatu ambayo ni ziara yake ya kwanza rasmi nchini humo ingawa amefanya ziara kadhaa za kikazi nchini Kenya.
Mama Salma Kikwete akiweka shada la maua kwenye Kaburi la Mwanzilishi wa Taifa la Kenya, Hayati Jomo Kenyatta jijini Nairobi Septemba 12, 2012 akiwa katika Ziara Rasmi ya Kiserikali (State Visit) ya siku tatu ambayo ni ziara yake ya kwanza rasmi nchini humo ingawa amefanya ziara kadhaa za kikazi nchini Kenya.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiweka jiwe la msingi katika jengo jipya la kutengeneza maziwa ya unga katika Kiwanda cha Maziwa cha Brookside Diary kwenye Barabara ya Thika nje kidogo ya jiji la Nairobi. Kushoto ni Mwenyekiti wa kampuni ya Brookside Diary Bw. Muhoho
Rais Kikwete akiangalia mchoro wa ujenzi wa jengo la kutengeneza maziwa ya unga wa kiwanda hicho. Anayemuelekeza ni Mwenyekiti wa kampuni ya Brookside Diary Bw. Muhoho Kenyatta,
Rais Kikwete akiangalia kondoo wanaofugwa kisasa katika shamba la kiwanda hicho
Rais Kikwete akiangalia ng'ombe wanaofugwa kisasa katika shamba la kiwanda hicho, n6- Rais Kikwete akiangalia kondoo wanaofugwa kisasa katika shamba la kiwanda hicho, n7- Rais Kikwete akiangalia mchoro wa ujenzi wa jengo la kutengeneza maziwa ya unga wa kiwanda hicho. Anayemuelekeza ni Mwenyekiti wa kampuni ya Brookside Diary Bw. Muhoho Kenyatta,
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wenyeji wake baada ya kutembelea Kituo cha Magonjwa ya Moyo na Kansa kwenye Hospitali ya Chuo Kikuu cha Aga Khan jijini Nairobi Septemba 12, 2012 akiwa katika Ziara Rasmi ya Kiserikali (State Visit) ya siku tatu ambayo ni ziara yake ya kwanza rasmi nchini humo ingawa amefanya ziara kadhaa za kikazi nchini Kenya.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akitembelea Chuo cha Taifa cha Ulinzi cha Kenya (National Defence College) kilichoko Karen, Nairobi,
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja n ujumbe wake na wanachuo na viongozi wa chuo hicho baada ya kukitembelea Chuo cha Taifa cha Ulinzi cha Kenya (National Defence College) kilichoko Karen, Nairobi, Picha na IKULU

Friday, September 7, 2012

MTANGAZAJI WA CLOUDS MEDIA GROUP BI SOPHIA KESSY AULA NAFASI YA UWAKILISHI UWT WILAYA YA MOSHI VIJIJINI...!!!

 
 
Mtangazaji mahiri wa kituo cha Radio na TV Clouds Media group cha jijini dare es saalam Bi Sophia Kessy .
---
UCHAGUZI WA JUMUIYA ZA CCM
Moshi (v) chaguzi zilianza rasmi tarehe 3/09 /2012 - 4/09/20121. Uvccm ulfanyika terehe 29/08/2012 mwenyekiti wake aliechaguliw ani Gulaton Masiga.2. Wazazi tarehe 03/09/2012 mwenyekiti wake ni sterwat lyatuu.3. UWT tarehe 04/09/2012 mwenyekiti wake ni Grace mzava

Aidha viongozi na wajumbe mbali mbali walichaguliwa na kupatikana chini ya uongozi wa chama wilaya ya moshi (V) Innocent Nzaba ni katibu wa ccm wilaya na mlezi wa jumuiya Gabriel Massenga ni mwenyekiti wa ccm wilaya,ambapo pia katika uchaguzi huo mtangazaji mahiri wa kituo cha Radio na TV Clouds Media group cha jijini dare es saalam Bi Sophia Kessy nae alijitosa katika uchaguzi huo kuwania nafasi ya uwakilishi wa UWT kwenda vijana wilaya na kuibuka mshindi kwa kura 415 dhidi ya kura zilizopigwa 416 ambapo kura 1tu iliharibika .
 
Bi Sophia kessy amesema kuwa kwa sasa ni hatua ndogo kati ya zile kubwa ambazo amepanga kujitosa na kuwania ambapo matarajio yake ya baadae ni kuwa kiogozi wa ngazi ya juu zaidi

Thursday, September 6, 2012

RAIS KIKWETE ATUNUKIWA TUZO YA UONGOZI BORA KATIKA SERA ZA KILIMO NA CHAKULA

 

 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikabidhiwa Tuzo ya Uongozi Bora wa sera ya Kilimo na Chakula toka kwa Bw. Ajay VAshee, Makamu Mwenyekiti wa asasi isiyo ya kiserikali inayohusika na sera za kilimo na chakula na Maliasili n ijulikanayo kama Food, Agriculture and Natural Resources Policy (FANRPAN) katika hoteli ya White Sands jana Septemba 5, 2012. Anayeshuhudia kulia ni Katibu Mtendaji wa FANRPAN) Dkt Lindiwe Sibanda. Tuzo hiyo, ambayo hutolewa kwa kiongozi aliyefanya juhudi kuhakikisha kuwepo kwa sera bora za kilimo na chakula nchini kwake, ilichukuliwa na Malkia Ntombi Indlovukazi wa Swaziland mwaka jana, wakati Rais Hifikepunye Pohamba alitunukiwa mwaka 2010, Rais Armando Emilio Gwebuza mwaka 2009 na Rais wa Malawi, Hayati Bingu Wa Mutharika, aliipokea mwaka 2008.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia baadhi ya ng'ombe anaowafuga kwa kufuata njia za kisasa kwenye shamba lake kijijini kwake Msoga, Chalinze, Wilaya ya Bagamoyo, leo Septemba 6, 2012

Wednesday, September 5, 2012

Michelle Obama amuombea mumewe kura

 
Mkewe rais Obama , Michelle akihutubia kongamano la Democrats
 
Mkewe Rais wa Marekani, Barack Obama, Michelle, amehutubia kongamano la chama tawala cha Democratic ambapo alitetea haki ya mumewe kupewa nafasi kutawala taifa hilo kwa muhula wa pili.
Akiongea Kaskazini mwa Jimbo la Carolina, alimtaja mumewe kama mtu anayeelewa matatizo yanayowakumba wamarekani.
Alitetea hatua ya mumewe ya kuanzisha mpango maalumu wa bima ya afya ulioleta utata mwingi sana hasa miongoni mwa wanachama wa chama cha upinzani cha Republican walioupinga.
Alisema kuwa mumewe alinuia kutoa nafasi sawa ya matibabu kwa wote. Hata hivyo alikiri kuwa mageuzi aliyoahidi mumewe miaka minne iliyopita yalikuwa magumu kuyatekeleza lakini akasisitiza kuwa yatafaulu baadaye.
Rais Obama atahutubia kongamano hilo baadaye juma hili, ambapo atakubali rasmi kuwa mgombea wa Urais wa chama cha Democratic.
 

Wednesday, August 29, 2012

KAHABA ATOA KICHAPO KIKALI KWA MLEMAVU ALIYE MDHULUMU 60,0000 AMBAYO ILIKUWA NI MALIPO YA USIKU MMOJA


VURUGU zilizuka nje ya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro kufuatia kahaba mmoja kumchapa makofi mlemavu wa miguu, Godlack Schone, 33, akimdai shilingi elfu 60 za ‘malipo’ ya huduma ya mapenzi aliyompa kwa usiku kucha.

Tukio hilo lilijiri wiki iliyopita mjini Morogoro na kuwalazimisha baadhi ya wafanyakazi wa mjengo huo kumjia juu changudoa huyo kwa kitendo cha kumpiga mlemavu mbele ya kadamnasi.

Akisimulia tukio hilo, karani mmoja wa ofisi hiyo anayefanya kazi upande wa utawala alisema chanzo cha ugomvi huo ni kahaba huyo kudai ‘haki’ yake baada ya kumpa ‘huduma’ ya mahaba Schone.

Kufuatia tukio hilo kubainika, hakuna mtu aliyekuwa tayari kumsaidia tena mlemavu huyo, hivyo alilala nje ya ofisi hiyo hadi siku iliyofuata ambapo alikwenda kwenye Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini, Mhe. Aziz Abood na kuomba msaada mwingine wa kurejeswa kwao ambapo alisaidiwa.

Tuesday, August 21, 2012

Director Tony Scott Commits Suicide, Jumps From Bridge



The director of 'Unstoppable', 'Top Gun''Beverly Hills Cop II', Tony Scott has committed suicide.

The 68 year old younger brother of popular movie director, Ridley Scott, jumped from the Vincent Thomas Bridge in San Pedro, California yesterday Sunday August 19th at about 12.30pm.Investigators from the Los Angeles Police Departmen found contact information in his car, which was parked near the bridge, and a suicide note in his office.A passerby who saw Scott jump from the bridge called 911. His body has been recovered from the water.Scott’s last film as a director was 2010’s Unstoppable. He is survived by his wife, Donna Wilson Scott, and their twin sons, Frank and Max.

Friday, August 17, 2012

MKUU WA MKOA WA DSM AHIMIZA SENSA YA WATU NA MAKAZI, ATOA ONYO KWA WALE WANAOENDESHA VITENDO VYA VURUGU


Na. Aron Msigwa -MAELEZO.
Dar es salaam.
Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya kuanza kwa zoezi la Sensa ya watu na makazi nchini, mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Saidi Meck Sadiki ametoa wito kwa wakazi wa mkoa huo kutoa ushirikiano kwa makarani wa sensa watakaoendesha zoezi hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam amesema maandalizi ya ukamilishaji wa zoezi hilo yanaendelea vizuri na kuongeza kuwa Waziri mkuu Mizengo Pinda anatarajia kuzindua kampeni ya uhamasishaji wa watu kushiriki katika zoezi hilo kesho (17/8/2012) katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.
Ametoa onyo na kuvitaka vikundi vya baadhi ya viongozi wa dini na wananchi wanaowahamasisha wananchi kutoshiriki katika zoezi hilo katika maeneo yao kuacha mara moja kwani zoezi hilo lipo kwa mujibu wa sheria namba 1 ya mwaka 2002.
"Natoa onyo kwa kikundi chochote kinachoendesha kampeni ya kuwahamasisha wananchi kutoshiriki kwenye zoezi la Sensa ya watu na makazi katika mkoa wa Dar es salaam kuacha mara moja kwani zoezi hilo lipo kwa mujibu wa sheria na yeyote atakayekaidi au kukwamisha zoezi hilo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake" amesema.
Amesema kuwa Zoezi la Sensa sio la mtu mmoja mmoja wala kikundi fulani bali ni suala la watanzania wote bila kujali dini, rangi wala kabila, hivyo watu wanaopinga zoezi hilo wanavunja sheria za nchi.
Naye mratibu wa zoezi la Sensa kwa mkoa wa Dar es salaam Bi. Magreth Stephen Mganda amesema mpaka sasa mkoa wa una jumla ya makarani na wasimamizi 18,993 watakaoshiriki zoezi la kuhesabu watu wakiwemo 90 wa akiba.
Amesema kati ya hao 644 wanatoka wilaya ya Kinondoni,365 wanatoka Ilala na 530 kutoka wilaya ya Temeke.
Katika hatua nyingine mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Bw. Saidi Meck Sadiki ametoa ufafanuzi wa vitendo vya vurugu,uharibifu na uporaji wa mali za wanachi katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Dar es salaam hususan wilaya ya Temeke na Kinondoni.
Amesema kuwa vitendo hivyo vilivyotokea ni kinyume cha sheria na kutoa onyo kwa wale wote waliohusika kuvamia maeneo na kuchukua ardhi kwa nguvu pasipo kufuata utaratibu kuacha mara moja.
Amesema kuwa wale waliovamia maeneo hayo bila kufuata utaratibu waondoke wenyewe na kukubali kutii sheria bila shuruti kwa kuwa serikali haitamvumilia mtu yeyote anayevunja sheria.
"Wale wote waliovamia maeneo hayo katika mkoa wa Dar es salaam katika maeneo yote yenye vurugu waondoke wenyewe , watii sheria kwa sababu vitendo vya namna hii ni vya kiharifu na kamwe serikali haiwezi kuvivumilia" amesisitiza.
Ameongeza kuwa tayari mahakama imeshatoa mwongozo kuhusu maeneo hayo na kubainisha kuwa wote waliohusika na watakaoendelea kuvunja sheria katika maeneo hayo watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Thursday, August 16, 2012

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI
















KAULI YA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KUHUSU MAJINA YA WALIOWEKA FEDHA USWIS.

.

Kambi rasmi ya upinzani bungeni imesema italazimika kuweka wazi taarifa na majina ya watu wenye umiliki wa fedha katika benki nchini Uswis zinazofikia bilioni 315.5 kama serikali haitatoa hizo taarifa.
Waziri kivuli na msemaji mkuu wa kambi rasmi ya upinzani bungeni Wizara ya fedha na uchumi Zitto Kabwe amesema hizo fedha zililipwa na makampuni ya utafutaji mafuta na gesi kwenye pwani ya mkoa wa Mtwara, kampuni ambazo zilipewa mikataba kati ya mwaka 2004 na 2006.
Nimemkariri Zitto akiongea bungeni kwamba “kambi rasmi ya upinzani bungeni imepata taarifa kuwa mmoja wa viongozi wa juu kabisa wa Tanzania na baadhi ya mawaziri wa serikali ya awamu zilizopita ni miongoni mwa wamiliki wa fedha hizi, sehemu kubwa ya fedha zililipwa na kampuni za utafutaji wa mafuta na gesi katika pwani ya mkoa wa Mtwara zilizopewa mikataba kati ya mwaka 2004 na 2006, kambi rasmi ya upinzani inaitaka serikali kutoa taarifa rasmi ya hatua gani ambayo imechukua mara baada ya kutolewa kwa taarifa kutoka benki ya taifa ya Uswis, tunaitaka serikali kuliambia taifa hatua itakazochukua kurejesha fedha hizi na nyingine zozote zilizofichwa ughaibuni”
Kuhusu ishu ya mjadala kuhusu kampuni ya BAE system ya Uingereza, Mh Zitto amesema “ukilinganisha fedha iliyorejeshwa kama chenchi ya rada na fedha ambayo Tanzania iliilipa benki ya Barclays, je chenchi ya rada ilikua na thamani yoyote kifedha? mjadala wa ununuzi wa rada hauwezi kuisha kwa kufurahia kurejesha chenchi tu, mjadala huu bado mbichi kabisa kwani tunataka ukweli mtupu uelezwe kwa umma na kuona taifa lilipata hasara kiasi gani kwa ufisadi huu wa kimataifa na hatua stahiki za kisheria kuchukuliwa dhidi ya wote walioliingizia taifa hasara”
Baada ya Zitto Kabwe kumaliza kuwasilisha, Mbunge wa Simanjiro (CCM) Christopher Ole Sendeka aliomba mwongozo kwa spika na kusema “tuhuma hii ni kubwa sana nilitaka kuomba mwongozo wako kwamba nani abebe mzigo huu, ni Zitto ataje majina ya wanaohusika au serikali iwataje hao wanaohusika katika utoroshaji wa fedha hizo ambazo zimeenda ughaibuni ili kila mmoja abebe msalaba wake pale itakapothibitika kwamba fedha za wananchi wa Tanzania zimepelekwa nje ya nchi bila kufata taratibu za kisheria

Tuesday, August 7, 2012

PICHA ZA AJALI YA NAIBU WAZIRI LEO.


.
.

.

     (Picha zimepigwa na francisgodwin.blogspot.com)
Naibu waziri wa Afrika Mashariki Abdullah Juma Saddallah amepata ajali ya gari alilokua akisafiria kwenye eneo la Kongowe Kibaha Pwani akitokea Dodoma kuja Dar es salaam.
Hiyo ajali imetokea leo jioni ambapo Naibu waziri amesema hali yake sio mbaya sana ila dereva ndio ameumia kiasi, bado wanapata matibabu kwenye hospitali ya Tumbi Kibaha Pwani,  chanzo cha ajali amesema ni baada ya dereva wake kukwepa lori lakini hakufanikiwa na gari ikatoka nje ya barabara.
                       
                       

Sunday, August 5, 2012

MWALIMU AFUKUZWA KAZI KWA KUONGEA "KISWAHILI" - ARUSHA

Mwalimu Daniel Urioh.
 Ninaomba WIZARA YA ELIMU iwe makini na wawekezaji katika secta ya elimu, hasa kwenye shule ambazo zinatoa msaada kwa watoto wakitanzania ambao familia zao hazina uwezo wa kifedha, kwa mfano ninaomba mmiliki wa shule ya St Jude apate muda wa kusikiliza kilio cha wafanyakazi wake wakitanzania kwani kimsingi wamekuwa wakiteswa, kukandamizwa na kupuuzwa wanapodai haki na maslahi bora kazini kwao.
Shule hii utumia picha za wafanyakazi kuzalisha kiasi kikubwa cha fedha kuendesha shule, kwa wafanyakazi na wanafunzi hupigwa picha mara kwa mara na kulazimishwa kuleta picha za familia zao kila mwaka bila shule kuweka wazi kwa mfanyakazi kuwa anawafadhili wangapi, wafadhili  huchangia kiasi gani cha fedha, kukatazwa kuwasiliana na mfadhili, kuruhusiwa kuhoji lolote kuhusu pato na matumizi ya uzalishwaji wa fedha kupitia wewe na familia yako? Hata hivyo picha za familia zinazalisha fedha kwaajili ya uendeshaji wa shule ilihali familia haifaidiki kwa uuzaji huo wa sura zao ughaibuni? Kinachosikitisha zidi ni pale mfanyakazi anapoachishwa ,shule inaendelea kitumia picha za wafanya kazi na familia zao kuzalisha fedha nyingi za kigeni bila ridhaa wala fedha hizo kuwafaidisha wenye picha, na kutojali kuwa kitendo hicho kinyume na sheria.  
 
Pia picha hizo zimekuwa mara kadhaa zikidhalilisha utu na uhuru wa muafrika, kwani sura za watanzania zimekuwa bidhaa ya kuzalisha fedha zisizojulikana ni kiasi gani na kwa faida ya nani? tena ulazimisha vitendo visivyo halisi na maisha yetu mfano unalazimishwa kucheka ukichukuliwa picha ilihali mapato uzalishayo hujui na ukikataa kutekeleza unatishiwa kufukuzwa kazi, wanafunzi ushikishwa zawadi zisikuwa zao na kupigwa picha na uzalisha kiasi cha fedha bila ridhaa wafunzi wanapohoji  hupewa adhabu au kutishiwa kufukuzwa.
 
Kama hiyo aitoshi shule hii imekuwa mara kadhaa ikipuuza sheria za nchi bila sababu za msingi mfano wamekuwa wakiajiri familia za ughaibuni kinyume na sheria za nchi mfano wanaajiri baba, mama na mtoto wa familia moja tena kwenye nafasi za juu na kutoweka wazi taaluma zao wakiwaaminisha kuwa ukiwa mzungu basi we msomi wa kila kitu, kinyume na sheria ya ajira nchini, pia shule imekuwa mara kadhaa haieshimu sikukuu za kitaifa bila sababu za lazima na kutojali wala kuthamini mchango wa waasisi na wazalendo waliopoteza maisha kujenga utaifa, amani na umoja wa Tanzania, cha kushangaza shule ujiamulia siku za mapumziko ya wafanyakazi na wanafunzi watakavyo wao, huwa najiuliza  hivi  shida inaweza tulazimisha kufuata sheria za wawekezaji na kupuuza sheria za nchi yetu Tanzania?
 
Linalosikitisha zaidi shule hii imekuwa hodari wa kupiga vita ya matumizi ya lugha ya kishwahili kwa wanafunzi na wafanyakazi hata kudiriki kuwaadhibu kwa kuwarudisha wanafunzi nyumbani kwa kosa la kuzunguza kishwahili, hata kufika mbali zaidi na kufukuza mwalimu mwenye shahada ya ualimu kwa kosa ni kuzungumza kishwahili na wanafunzi, huu ni uvunjaji wa sheria za nchi usiovumilika.
Hata hivyo nataka wao wajue kuwa lugha ya taifa Kiswahili imekuwa mhimili mkubwa wa kujenga umoja na amani. Kiasi cha kuwa wekeza kupata mafanikio, kama awa amini wakajaribu kuwekeza Somalia na kuwasaidie watoto wa Somalia wenye shida kubwa ya elimu, ilo linge ondoa jeuri yao ya kupuuza sheria za Tanzania.
Kitendo cha shule hii kuwatumia watanzania kama bidhaa na utaratibu wao wa fukuza fukuza waliyonayo hasa kwa watanzania.  Shule hii huwatumia viongozi wazalendo kuwanyanyasa wenzao na kusaidia shule kuendelea na  dharau na kupuuza sheria za nchi zenye maslahi kwa wazalendo, wale wote watakaonyesha uzalendo kama mimi wakuonyesha kukerwa na kuchukua hatua ya kuhoji na kutetea sheria za nchi na watanzania dhidi ya upuuzwaji wa uzalendo, haki, utu, lugha ya taifa, maslahi ya kiwango cha utumikishwaji, niliishia kufukuzwa kwa kosa la kuongea kishahili na wanafunzi.
 
Ushauri wangu kwa wizara ya elimu.
Kwanza kupandisha mshahara na mazingira ya kazi serikalini ilikuvutia waalimu wote toka shule binafsi kwani wangi wamechoshwa ni manyanyaso ya waajiri.
Pili kufanya ukagua si wa taaluma tu bali pia mfumo wa uajiri na maslahi ya watanzania waajiriwa kwenye shule zinazomilikiwa binafsi kwa misaada ya watu toka ughaibuni.
Tatu iwe na utaratibu wa ufuatiliaji wa mapato na matumizi ya shule zinazopata fedha toka kwa wafadhili kwani shida za  watanzania zimekuwa zikinufaisha wachache na kutengeneza ajira ya watu wasiona sifa za kufanya kazi ughaibuni na kuja kufanya kazi ambazo wazalendo wanaweza kuzifanya.
Nne kusisitiza hasa shule binafsi nchini kuthamini lugha ya kishwahili, kuheshimu sheria za ajira, kuheshimu sikukuu za kitaifa na kuheshimu, kulinda tamaduni  na vipaji vya watanzania kwa manufaa ya Tanzania. 
 
Ni kweli tar 15/06/2012 nimefukuzwa kazi ya kufundisha (ualimu) St-Jude-Arusha kwa kosa la kuzungumza Kiswahili. 
 
Uzalendo gharama nimeamua kujitoa kwa kutetea nchi yangu Tanzania.
 
Mwalimu Daniel Urioh. Kwa undani zaidi piga :+255 755 379 737.

                                                      CHANZO NA kajunason.
 

Saturday, August 4, 2012

Mwanafunzi amchoma kisu mwalimu wake!!


Mwanafunzi wa kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari ya Mbondole, Kata ya Msongola, Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam, Neneu Baltazar, anatuhumiwa kuchoma kisu mwalimu wake, Frank Gama, baada ya kuzuka vurugu shuleni hapo.

Vurugu hizo zilitokea baada ya mwanafunzi wa kike kuibiwa simu yake ya kiganjani na kumhisi mwanafunzi mwenzake Neneu kuwa ndiye aliyehusika na wizi huo.

Hata hivyo, Neneu alipokataa, ndipo vurugu zilipoibuka kati ya wanafunzi hao wawili.

Akisimulia mkasa huo, Mwalimu Gama alisema baada ya kuona wanafunzi hao wanagombana, alichukua jukumu la kwenda kuamulia ugomvi huo.

Hata hivyo, alisema wakati akifanya hivyo, ghafla alijikuta akichomwa kisu mgongoni.

“Vijana hao wamenipiga sana lakini isingekuwa walimu wenzangu kuja kuniokoa, sijui ingekuwaje. Kwani walikuja kama nyuki nimeumizwa na sasa nakwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili kutibiwa,” alisema Mwalimu Gama.

Makamu wa Mkuu wa shule hiyo, Juma Robinson, aliliambia NIPASHE jana kuwa vurungu hizo zilisababishwa na utovu wa nidhamu wa wanafunzi wa shule hiyo.

Alisema vurugu kama hizo za kupigwa walimu shuleni hapo, ni jambo la kawaida kwani hata yeye aliwahi kupigwa ngumi lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa.

Hata hivyo, Juma alisema tukio hilo la jana walitoa taarifa  polisi jamii wa mtaa huo ambao walifika na kumkamata mmoja wa wanafunzi hao lakini wengine walikimbia. 

“Utovu wa nidhamu katika shule za kata zinasababishwa na kutokuwa na bodi za shule na maamuzi katika kila shule huachiwa mtu mmoja," alisema. 

Kamanda wa Polisi Jamii katika mtaa huo, Richard Mosoba, alisema walipofika eneo hilo, walimkamata mwanafunzi huyo na kumfikisha katika kituo cha  Polisi cha Stakishari Ukonga.

“Sisi tulijitahidi kutimiza jukumu letu la kumfikisha mtuhumiwa aliyemchoma kisu mwalimu, lakini nini kitafuatia, hiyo ni kazi ya polisi. Kwanza hatuna silaha zaidi ya pingu, sasa unategemea nini kitokee kwenye vurugu?,” Alihoji Mosoba.

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Ilala, Marietha Minandi, alithibisha kutokea kwa tukio hilo.

Alifafanua kuwa ugomvi huo uliwahusu wanafunzi na kidato cha tatu na cha nne baada ya mwanafunzi mmoja kuibiwa simu na kumhisi wa kidato cha nne kuwa ndiye aliyeiba.

Alisema wanafunzi walipigana na baadhi yao wakamua kumuita mwalimu aende kuwaamulia lakini alipofika mwanafunzi mmoja alichoma kisu.

Mwanafunzi huyo kwa sasa anamshikiliwa polisi kwa kwa mahojiano.

CHANZO: KULIKONI

Saturday, July 28, 2012

'I would knock her teeth out if she spoke to me like that': Jackson family friend Gladys Knight lashes out at Paris for mouthing off at aunt Janet


Gladys Knight has weighed into the Jackson family feud - insinuating 14-year-old Paris needs to pipe down and learn some respect for her elders.
The 68-year-old soul singer - who is a friend of the famous clan - said she would have knocked the teen's teeth out if she had spoken to her like she did to Janet during Monday's altercation at the Calabasas compound.
Paris is said to have had an explosive argument with her 46-year-old aunt Janet on Monday as tensions heightened over matriarch Katherine's whereabouts.
Old fashioned approach: Gladys Knight appeared on CBS's The Talk this morning, saying she was appalled at the way Paris spoke to aunt Janet during a row at the Jackson house this week
Old fashioned approach: Gladys Knight appeared on CBS's The Talk this morning, saying she was appalled at the way Paris spoke to aunt Janet during a row at the Jackson house this week
Janet apparently called Paris a 'spoiled little b****' while Paris shot back: 'This is our house. Not the Jackson family house. Get the f*** out!' 
Now Gladys - known as The Empress of Soul - has made her loyalties clear.
Speaking on U.S. daytime show The Talk, she fumed: 'You've got to understand Paris is 14? How old is Janet? Who's the one to try to direct the other one here? I would think it's a good thing [Janet] lets Paris know who she is.'
She went on: '[Janet] is just trying to protect her in a way. But if she [Paris] called me that she would have no teeth.'
Show some respect: The soul singer said Paris should not talk badly to her elders
Show some respect: The soul singer said Paris should not talk badly to her elders
Show some respect: The soul singer said Paris should not talk badly to her elders
Forthright: Knight said she would have knocked out Paris' teeth if she had spoken rudely to her
Forthright: Knight said she would have knocked out Paris' teeth if she had spoken rudely to her
Gladys earlier explained: 'I was raised in the southern way,' adding later in the interview: 'That's the way we were brought up. You respect your elders.'
The interview comes as Michael Jackson's mother Katherine and her nephew TJ Jackson are both expected to file court documents this morning to share custody of Jacko's three children, Prince, Paris and Blanket.
The pair met last night in the company of lawyers to hash out an agreement over the care of the siblings, aged 10 to 15.
A judge granted Tito Jackson's son TJ temporary guardianship on Wednesday, citing concerns that Katherine was being prevented from fulfilling her role as guardian 'by a third party' following her days-long absence from the California home she shares with the children.
Feud: Paris remonstrates with Janet at the Jackson Calabasas compound earlier this week. Janet called Paris a 'spoiled little b****' while Paris shot back: 'This is our house. Not the Jackson family house. Get the f*** out!'
Feud: Paris remonstrates with Janet at the Jackson Calabasas compound earlier this week. Janet called Paris a 'spoiled little b****' while Paris shot back: 'This is our house. Not the Jackson family house. Get the f*** out!'
Drama: The Jackson family feud has reached boiling point this week after matriarch Katherine went AWOL
Drama: The Jackson family feud has reached boiling point this week after matriarch Katherine went AWOL
Drama: The Jackson family feud has reached boiling point this week after matriarch Katherine went AWOL


                                   Source: http://www.dailymail.co.uk/tvshowbiz/article-2179974/Gladys-Knight-lashes-Paris-mouthing-aunt-Janet.html#ixzz21uVWXjdq

Thursday, July 26, 2012

Wajue Wanawake 5 shupavu Afrika



Ellen Johnson-Sirleaf, rais wa Liberia ana umri wa miaka, 72 na alitajwa kama mshindi wa tatu wa tuzo ya Amani ya Nobel mwaka 2011. Tuzo hiyo imetolewa miaka sita baada ya yeye kuchaguliwa rais wa Liberia na kumfanya kuwa rais wa kwanza mwanamke barani Afrika.



Joyce Banda, rais wa Malawi. Bi Banda mwenye umri wa miaka 62, amefanya jambo la kihistoria kwa kuwa rais wa kwanza mwanamke nchini humo. Pia yeye ni mwanamke wa pili kuongoza nchi ya ya kiafrika. Anaheshimika kama mwanaharakati wa haki za wanawake.

 

Nkosazana Dlamini-Zuma, Mwenyekiti wa Tume ya Muungano wa Afrika. Alichaguliwa tarehe kumi na tano mwezi Julai baada ya kinyang'anyiro kikali kati yake na mwenyekiti wa zamani Jean Ping. Bi Dlamini-Zuma, mwenye umri wa miaka 63, ni mwanamke wa kwanza kuwahi kushikilia wadhifa huo.



Ngozi Okonjo-Iweala, Waziri wa fedha wa Nigeria. Bi Okonjo-Iweala, mwenye umri wa miaka 58, ameshikilia nyadhifa mbalimbali za kimataifa, katika sekta ya fedha .Aliheshimika sana wakati akiwa Mkurugenzi Mkuu katika Benki ya Dunia kwa miaka mitatu, kabla ya kushindana katika kinyang'anyiro kuwa Rais wa benki hiyo.


Fatou Bensouda, Mwendesha Mkuu wa Mashtaka katika Mahakama ya kimataifa ya jinai, ICC. Bensouda mwenye umri wa miaka 51, aliteuliwa katika wadhifa huo mwezi Juni mwaka huu na kuchukua nafasi ya Luis Moreno-Ocampo kutoka Argentina. Kabla ya hapo Bensouda alikuwa naibu mwendesha mkuu wa mashtaka tangu mwaka 2004.


Chanzo - BBC Swahili